“NILIVULIWA NGUO NIKABAKI MTUPU MAKABURINI” - MAYE


JUMANNE , 29TH SEP , 2020

Mtangazaji wa kipindi cha Dadaz ya East Africa TV Maye Kidoti amesema amewahi kujihusisha na masuala ya kishirikina na kufikia hatua hadi ya kwenda kwa mganga ili mradi awe maarufu lakini ikashindikana.

Mtangazaji Maye Kidoti

Akizungumza hayo wakati wanajadili mada ya kipi kinasababisha watu kwenda kwa waganga Maye Kidoti amesema yeye amewahi kwenda kwa mganga na akafuata masharti ya kubaki mtupu makaburini lakini bado hajafanikiwa.

" Nilishawahi kwenda kwa waganga na nishavuliwa nguo nikabaki mtupu huku mganga alikuwa ananiona na kunizungusha kwenye kaburi ambalo nilikuwa sijui la nani, kilichonipeleka kwa mganga ulikuwa ni ujinga wa kutafuta umaarufu na sikuupata mpaka nilipoachana na hayo mambo na kuamua kuokoka" amesema Maye Kidoti
" Pia n ilishaenda kwa waganga wa vitabu na bado wakanipa nazi kuvunja njia panda, hii hali ya kupewa nazi kupeleka njia panda ni sawa na uchawi tu kwa sababu unajikuta unamshirikisha Mungu mambo ya waganga sio sawa, asikwambie mtu waganga ni waganga tu hakuna wa kutibu wala wa tunguli " ameongeza
eatv.tvSep 29, 2020

No comments

Powered by Blogger.